ISIKUPITE

Blogroll

Sunday, 7 October 2018

Hizi hapa, FAIDA 20 ZA KUTEMBEA KAMA SEHEMU YA MAZOEZI


Kutembea ni njia salama na nzuri inayosaidia kuujenga na kuuimarisha moyo uwe na afya nzuri na usio katika hatari ya kushambuliwa na maradhi.
Mazoezi au tabia ya kufanya mazoezi ya kutembea inayo faida kubwa zaidi kuliko matumizi ya dawa.
  1. Mazoeziya kutembea husaidiakupunguza uzito, tembea dk 60 kila siku
  2. Ni mazoezi yanayoweza kufanywa na kila mtu
  3. Ni mazoezi yasiyohitaji vifaa (hayana gharama)
  4. Ndiyo njia rahisi kabisa ya kuufanya mwili kuwa mkakamavu
  5. Hupunguza dalili za majonzi na wasiwasi
  6. Ni mazoezi yenye matokeo ya taratibu
  7. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na kolesto (lehemu)
  8. Hupunguza na kutibu shinikizo la damu
  9. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na baadhi za kansa
  10. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na kisukari
  11. Hukufanya ujisikie vizuri
  12. Husaidia kuimarisha mifupa
  13. Husaidia kupunguza uwezekano wa kupatwa na shambulio la moyo
  14. Ni mazoezi uwezayo kuyafanya bila kukusababishia ajari au maumivu makubwa
  15. Hupunguza mfadhaiko (stress)
  16. Hupunguza uwezekano wa kupatwa na ugonjwa wa moyo
  17. Ni mazoezi unayoweza kuyafanya bure bila kulipia chochote
  18. Husaidia kuimarisha mishipa
  19. Husaidia katika mfumo wa upumuwaji
  20. Husaidia kuongeza mzunguko wa damu
Kama afya yako siyo nzuri sana anza kutembea kidogo kidogo labda dakika 10 kwa siku huku ukiongeza dakika 5 kila siku hadi hapo utakapoweza kutembea lisaa limoja mfululizo bila kupumzika.
Ili kupunguza uzito, unene, utipwatipwa, mafuta yaliyozidi au kitambi, fanya zoezi la kutembea kwa miguu mwendo kasi kidogo lisaa limoja kila siku muda wa mwezi mmoja mpaka miwili mfululizo.
Je ni muda gani mzuri wa kufanya mazoezi ya kutembea?,
Wengi wanapenda asubuhi sana na jioni lakini mimi napenda kufanya mazoezi ya kutembea mchana wakati wa jua kali saa sita, saa saba au saa nane, tena huwa natoa kabisa shati na kubaki tumbo wazi.
Utanishangaa kwanini nafanya hivi!, Jua lina umhimu sana kwa afya ya mwili na ngozi pia kama chanzo cha vitamini D, vitamini ambayo ni mhimu sana katika kuimarisha mifupa na hivyo kuzuia ugonjwa wa mifupa (osteoporosis), kuzuia maumivu ya mishipa, kushusha shinikizo la juu la damu, kudhibiti kisukari, kudhibiti kolesto na kadharika.
Unapotembea mchana wa jua kali unaruhusu jua kutua juu yako mwili mzima.
Unajisikia aibu kutembea nje barabarani? au unakosa muda kabisa kwenda kiwanjani kwa ajili ya mazoezi ya kutembea? Kama ni hivyo basi unaweza kununua mashine ya kutembea inayotumia umeme na ukaifunga chumbani kwako na ukawa unajifanyia mazoezi huko huko chumbani kwako, mashine inaitwa ‘TreadMill’.  Iangalie kwenye picha hapa chini au namna inavyotumika kwenye video hapo chini zaidi;


No comments:

Post a Comment